Nitakutukuza Mungu
| Nitakutukuza Mungu | |
|---|---|
![]() | |
| Alt Title | Kwa Kinywa Changu |
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) |
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) |
| Category | Thanksgiving / Shukrani |
| Composer | S. E. Mlugu |
| Video | Watch on YouTube |
| Views | 7,397 |
Nitakutukuza Mungu Lyrics
Kwa kinywa changu Mungu wangu nitakutukuza,
kwa nyimbo nzuri nitaziimba sifa (zako )
Kwa kuwa Mungu wema wako kwangu mimi ni mkuu siwezi kuelezea
{ Sina kitu Bwana cha kukupa (wewe)
kulingana na mema uloyatenda
Naitoa kwako nafsi yangu (Bwana)
nitendee unavyotaka } *2- Kama ni pumzi ya uhai umenipa bure,
Sauti nzuri ya kuimbia, yatoka kwako
Nakurudishia sifa na shukrani - Kama ni elimu, niliyo nayo ni mali yako,
Ujuzi na kazi niliyo nayo vyatoka kwako
Nakurudishia sifa na shukrani - Magonjwa mengi umeniponya ee Mungu wangu,
Na ajali nyingi umenikinga ee Mungu wangu
Nakurudishia sifa na shukrani
