Nitakutukuza Mungu
| Nitakutukuza Mungu | |
|---|---|
|  | |
| Alt Title | Kwa Kinywa Changu | 
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | S. E. Mlugu | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 7,365 | 
Nitakutukuza Mungu Lyrics
- Kwa kinywa changu Mungu wangu nitakutukuza,
 kwa nyimbo nzuri nitaziimba sifa (zako )
 Kwa kuwa Mungu wema wako kwangu mimi ni mkuu siwezi kuelezea
 { Sina kitu Bwana cha kukupa (wewe)
 kulingana na mema uloyatenda
 Naitoa kwako nafsi yangu (Bwana)
 nitendee unavyotaka } *2
- Kama ni pumzi ya uhai umenipa bure,
 Sauti nzuri ya kuimbia, yatoka kwako
 Nakurudishia sifa na shukrani
- Kama ni elimu, niliyo nayo ni mali yako,
 Ujuzi na kazi niliyo nayo vyatoka kwako
 Nakurudishia sifa na shukrani
- Magonjwa mengi umeniponya ee Mungu wangu,
 Na ajali nyingi umenikinga ee Mungu wangu
 Nakurudishia sifa na shukrani
 
  
         
                            