Nitakutukuza Mungu

Nitakutukuza Mungu
Alt TitleKwa Kinywa Changu
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumAsifiwe Bwana Mungu (Vol 8)
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerS. E. Mlugu
VideoWatch on YouTube
Views6,295

Nitakutukuza Mungu Lyrics

  1. Kwa kinywa changu Mungu wangu nitakutukuza,
    kwa nyimbo nzuri nitaziimba sifa (zako )
    Kwa kuwa Mungu wema wako kwangu mimi ni mkuu siwezi kuelezea
    { Sina kitu Bwana cha kukupa (wewe)
    kulingana na mema uloyatenda
    Naitoa kwako nafsi yangu (Bwana)
    nitendee unavyotaka } *2

  2. Kama ni pumzi ya uhai umenipa bure,
    Sauti nzuri ya kuimbia, yatoka kwako
    Nakurudishia sifa na shukrani
  3. Kama ni elimu, niliyo nayo ni mali yako,
    Ujuzi na kazi niliyo nayo vyatoka kwako
    Nakurudishia sifa na shukrani
  4. Magonjwa mengi umeniponya ee Mungu wangu,
    Na ajali nyingi umenikinga ee Mungu wangu
    Nakurudishia sifa na shukrani