Natazama Kalvari

Natazama Kalvari
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumAsifiwe Bwana Mungu (Vol 8)
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerGabriel Kapungu
Views5,651

Natazama Kalvari Lyrics

  1. Nimekukosa Bwana, kwa moyo wote ninajuta kweli, kwa moyo wote
    Roho yangu ina-yohuzunika ninapokuona ulivyokufa

    { Natazama Kalvari (Bwana) ulivyotundikwa mtini (kweli)
    Mwili wangu wanyong'onyea ulivyosulibiwa } *2

  2. Tena ni mimi Bwana, ni dhambi zangu ulizozifia, msalabani
    Kifo cha aibu, kilikufika makusudi mimi, niokolewe
  3. Kwenye kilima kile, walikusonya wakisema wote, asulibiwe
    Kifo chako kwetu ni ukombozi wa mioyo yetu, na roho zetu
  4. Unitulize Bwana, kwa mkono wako kwani ninatubu, makosa yangu
    Naanguka kwako kifudifudi, ninaomba toba, kwa moyo wote