Natazama Kalvari
| Natazama Kalvari | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | Gabriel Kapungu | 
| Views | 6,689 | 
Natazama Kalvari Lyrics
- Nimekukosa Bwana, kwa moyo wote ninajuta kweli, kwa moyo wote
 Roho yangu ina-yohuzunika ninapokuona ulivyokufa{ Natazama Kalvari (Bwana) ulivyotundikwa mtini (kweli)
 Mwili wangu wanyong'onyea ulivyosulibiwa } *2
- Tena ni mimi Bwana, ni dhambi zangu ulizozifia, msalabani
 Kifo cha aibu, kilikufika makusudi mimi, niokolewe
- Kwenye kilima kile, walikusonya wakisema wote, asulibiwe
 Kifo chako kwetu ni ukombozi wa mioyo yetu, na roho zetu
- Unitulize Bwana, kwa mkono wako kwani ninatubu, makosa yangu
 Naanguka kwako kifudifudi, ninaomba toba, kwa moyo wote
 
  
         
                            