Asifiwe Bwana Mungu

Asifiwe Bwana Mungu
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumAsifiwe Bwana Mungu (Vol 8)
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerF. S. Matemele
Views6,141

Asifiwe Bwana Mungu Lyrics

  1. { Asifiwe Bwana Mungu aliyeumba mbingu na nchi (na nchi)
    Asifiwe katika patakatifu ( pake)
    Enzi na utawala wake (wa milele)
    Asifiwe kwa matendo (matendo) yake makuu} *2
    { Kageuza bahari kuwa nchi kavu
    ( na pia) ametoa maji - kwenye mwamba
    (Na tena) amewalisha watu - kwa mana kama Mungu } *2
    { Asifiwe yeye kwa matendo yake (hayo) makuu } *2

  2. Asifiwe, Yeye kwa kuwa, ni Bwana wa nguvu,
    Na hodari hodari wa vita, nguvu zake zapasua milima
    { Asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana)
    Milele (milele) milele (milele)
    Milele (milele) milele (milele)
    Asifiwe Bwana na nguvu zake (tumpe)
    Sifa na heshima ni vyake (ee mfalme) hata milele } *2
  3. Asifiwe yeye kwa kuwa ni Bwana wa mabwana
    Na mfalme mfalme wa wafalme,na mamlaka zatawaliwa naye
    { Asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana)
    Milele (milele) milele (milele)
    Milele (milele) milele (milele)
    Asifiwe Bwana na nguvu zake (tumpe)
    Sifa na heshima ni vyake (ee mfalme) hata milele } *2
  4. Asifiwe Yeye kwa kuwa ni mume wa wajane,
    Na Baba wa walio yatima, upendo wake hauna mipaka
    { Asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana), asifiwe (Bwana)
    Milele (milele) milele (milele)
    Milele (milele) milele (milele)
    Asifiwe Bwana na nguvu zake (tumpe)
    Sifa na heshima ni vyake (ee mfalme) hata milele } *2
edited by John Kasindi (JOKA)