Apewe Sifa
   
    
     
         
          
            Apewe Sifa Lyrics
 
             
            
- { Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee heee
 Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee hee } *2
 
 
 { Utukufu nakupa wewe, utukufu nakupa wewe,
 Sifa na heshima nakupa we,
 Ewe mwenyezi unaweza } *2
 
- Nguzo ya moto aliwasha, nilindwe usiku,
 Nayo ya wingu akashusha nipite mchana
 Nakumbuka mapito yote, niliyopitia,
 Nakumbuka na njia zote, nilizopitia
 
 Tazama Mungu tazama wewe,
 Tazama Mungu tazama wewe
 Tazama Mungu tazama wewe unatimiza ahadi yako
 Tazama Mungu tazama wewe,
 (tazama Mungu ) ni mwaminifu
 Tazama Mungu tazama wewe unatimiza ahadi yako
 
 Utukufu nakupa . . .
- Jemedari mwenye maguvu, yule Goliathi,
 Akamlaza kwa kombeho, mkononi mwangu
 Nakumbuka alikemea, mawimbi ya maji,
 Nakumbuka yalimtii, nikafika ng'ambo
 Tazama Mungu tazama . . .
 
 Utukufu nakupa . . .
 
 ~ ~ ~
 a) Bahari haiwezi kutuzuia -
 Tunatembea bila mitumbwi
 Na maji yanageuka kuwa ukuta -
 Mungu mwenyewe ni mtumbwi wetu tunavuka
 
 b) Maana amesema tumfuate -
 Mizigo itulemeayo tukampe -
 
 c) Muhimu tumwendee tukiamini -
 Na hata juu ya maji tutakanyagaa -
 
 ~ ~ ~
 { Alimkumbuka Daudi mtumishi wake
 Akamkweza akawavusha waisrael
 katika maji bila mitumbwi } *2
 
 Apewe, apewe, apewe sifa kuu
 Mungu apewe, apewe, milele milele
 Apewe apewe, apewe sifa kuu
 Mungu apewe, apewe
 Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee hee