Apewe Sifa

Apewe Sifa
Alt TitleSifa na Utukufu
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMimina Neema
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerZacharia Gerald
Views48,420

Apewe Sifa Lyrics

  1. { Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee heee
    Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee hee } *2


    { Utukufu nakupa wewe, utukufu nakupa wewe,
    Sifa na heshima nakupa we,
    Ewe mwenyezi unaweza } *2

  2. Nguzo ya moto aliwasha, nilindwe usiku,
    Nayo ya wingu akashusha nipite mchana
    Nakumbuka mapito yote, niliyopitia,
    Nakumbuka na njia zote, nilizopitia

    Tazama Mungu tazama wewe,
    Tazama Mungu tazama wewe
    Tazama Mungu tazama wewe unatimiza ahadi yako
    Tazama Mungu tazama wewe,
    (tazama Mungu ) ni mwaminifu
    Tazama Mungu tazama wewe unatimiza ahadi yako

    Utukufu nakupa . . .
  3. Jemedari mwenye maguvu, yule Goliathi,
    Akamlaza kwa kombeho, mkononi mwangu
    Nakumbuka alikemea, mawimbi ya maji,
    Nakumbuka yalimtii, nikafika ng'ambo
    Tazama Mungu tazama . . .

    Utukufu nakupa . . .

    ~ ~ ~
    a) Bahari haiwezi kutuzuia -
    Tunatembea bila mitumbwi
    Na maji yanageuka kuwa ukuta -
    Mungu mwenyewe ni mtumbwi wetu tunavuka

    b) Maana amesema tumfuate -
    Mizigo itulemeayo tukampe -

    c) Muhimu tumwendee tukiamini -
    Na hata juu ya maji tutakanyagaa -

    ~ ~ ~
    { Alimkumbuka Daudi mtumishi wake
    Akamkweza akawavusha waisrael
    katika maji bila mitumbwi } *2

    Apewe, apewe, apewe sifa kuu
    Mungu apewe, apewe, milele milele
    Apewe apewe, apewe sifa kuu
    Mungu apewe, apewe
    Sifa na utukufu vyote ni kwa Mungu hee hee