Niruhusu ee Yesu

Niruhusu ee Yesu
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
ComposerE. F. Kidaluso
Views34,106

Niruhusu ee Yesu Lyrics

  1. Niruhusu Yesu wangu, niijongee meza yako
    Unisamehe dhambi Mwokozi,
    uje rohoni mwangu uniokoe
    Njoo kaa ndani yangu, nami nikae ndani yako
    Ili nipate amani tele, ndani ya Roho yangu nifarijike

    { Wewe Bwana (wewe Bwana wanijua)
    Wanijua (hata nafsini mwangu)
    Wewe ndiwe tabibu pekee wa roho yangu
    Tena ndiwe kimbilio langu }*2

  2. Tazama Yesu wangu ninajongea karamu yako
    Pengine kwako Bwana sikustahili kuijongea
    Unihurumie ee Yesu wangu unisamehe
  3. Hakika kwako Bwana makosa mengi nimeyatenda
    Ubinadamu wangu siwezi kuficha kwako Bwana
    Unihurumie ee Yesu wangu unisamehe
  4. Niwazi Yesu wangu unaujua udhaifu wangu
    Sina chakujitolea mbele yako Ee Yesu wangu
    Unihurumie Ee Yesu wangu unisamehe