Nusu kwa Nusu

Nusu kwa Nusu
Alt TitleMungu Alivyo
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMimina Neema
CategoryTafakari
ComposerD. Nkoko
Views15,280

Nusu kwa Nusu Lyrics

  1. Ni yule yulee
    Ni yule yulee
    Ni yule yulee

    Mungu alivyo ooh hivyo ndivyo alivyo,
    Mungu alivyo ooh hivyo ndivyo alivyo,
    Mchana ni yule yule ( na ) usiku ni yule yule,
    (Yeye) habadiliki ni yule, daima ni yule yule,
    ( ye ni yule Mungu) Mungu alivyo ooh
    Hivyo ndivyo alivyo ndivyo alivyo

  2. Alifundisha upendo akawafia wadhambi
    Kahubiri msamaha kaombea wauaji
    Anahimiza amani hata kwa wanaomkamata
    Kweli Mungu habadiliki (yeye) ni yule yulee
  3. Kaagiza ubatizo akabatizwa mwenyewe
    Alihubiri huruma akawaponya wakoma
    Anahimiza ibada naye hakutegea kusali
    Kweli Mungu habadiliki (yeye) ni yule yulee

    ~ ~ ~

    Lakini mwanadamu mimi- Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu *2

    Nahubiri upendo - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Huku nateta wenzangu - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Nataka msamaha - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Huku nashitaki watu - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Natangaza amani - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Huku nabeba silaha - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Navaa msalaba - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Na hirizi kiunoni - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Nina pete ya ndoa - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Na hawara mafichoni - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Napaswa kugeuka - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu
    Niwe mwenye msimamo - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu

    Maana mwanadamu mimi - Mwanadamu mimi ni nusu kwa nusu *3