Nyota ya Mashariki
   
    
     
         
          
            Nyota ya Mashariki Lyrics
 
             
            
- Kakukirimia, uwe ulivyo,
 Atakutumia impendezavyo
 Akikuinua, inuka, hivyo,
 Ninakuombea heri vilivyo;
 
 Hakunipa hayo, nikuhitaji,
 Kwa niliyo nayo, upate maji,
 Na mwisho wa hayo, tuvikwe taji,
 Tuingie nayo, wa mbingu mji.
 { Nimeiona nyota yako mashariki (nyota yako)
 Ninajivuna inavyong'ara rafiki (helelelele)
 Naandamana kuja unakotamalaki
 Kumsujudia Bwana aliyekupa milki (ho ndugu) } *2
- Sirudi kwa njia, yake herode,
 Anakuvizia, kila upande,
 Wivu unamjia, kakunja, konde,
 La kukuzuia juu usipande;
 
 Ni kama Kaini, mwua Abeli,
 Au Raubeni, wa Israeli,
 Waliotamani, kuzika, hali,
 Ya wadogo duni, wake Jalali!
- Ninakuombea, usife moyo,
 Maana dunia, si rafikiyo,
 Wewe fuatia, za Kristu, nyayo,
 Aliyekufia, kwa mizigoyo;
 
 Wa ulimwenguni, watakufumba,
 Wazuri machoni, moyo mwembamba,
 Hawatatamani, uitwe, mwamba,
 Ni wivu moyoni, unawasomba!