Nitakutukuza Mungu

Nitakutukuza Mungu
Alt TitleUhimidiwe
Performed by-
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerZacharia Gerald
Views7,553

Nitakutukuza Mungu Lyrics

  1. Bwana viumbe vyote vilivyoumbwa nawe
    Vinakutukuza kwa haki *2
    Ona mimea nayo iliyoumbwa nawe
    Inakutukuza kwa haki, inakutukuza Mungu

    Uhimidiwe Baba yetu uhimidiwe
    Uhimidiwe uhimidiwe
    Uhimidiwe Baba yetu uhimidiwe
    Uhimidiwe Mungu upewe sifa

  2. Bahari na vitu vyote viliyoumbwa nawe
    Vinakuimbia kwa haki *2
    Ona dunia yote iliyoumbwa nawe
    Inakuimbia kwa haki, inakuimbia Mungu
  3. Bwana nikiyatazama matendo yako kwangu
    Ninakutukuza kwa haki
    Ninakutukuza ee Mungu
    Ninakosa la kusema, ni mengi mno kwangu
    Ninakushukuru ee Yesu, ninakushukuru sana
  4. Mfalme Daudi alikuchezea - uhimidiwe
    Na mavazi yake kayararua - upewe sifa
    Mimi ni nani nisikutukuze -uhimidiwe
    Nitakuimbia ningali hai - upewe sifa
    Wafalme nao wanakutukuza - uhimidiwe
    Na majeshi yote yanakusifu - upewe sifa
    Kwa kinywa changu napaza sauti - uhimidiwe
    Na nyumba yangu wote tunasema - upewe sifa

    Upewe sifa, upewe sifa *2
    Nitakusifu milele milele (Baba) milele *8