Mtume

Mtume
Alt TitleNitamwimbia Bwana Milele
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views8,196

Mtume Lyrics

  1. Dunia hii ni ngumu sana
    Yenye mapito mazito
    Siku zote watu kulumbana
    Kote kote kuna moto
    Ooo ni vigumu mno
    Ooo kuwajibika
    Kwa aliyekutuma
    Lakini mimi, tazama

    Nimeinua macho yangu
    Nimtazame mmoja
    Yeye ni rafiki yangu
    Kisiwa cha faraja
    Mimi ni mtume wake
    Mtume wa uimbaji
    Ninaimba nyimbo zake
    Kwa wanaomhitaji Yesu

  2. Duniani kumejaa wivu
    Ugombea utukufu
    Hasira kali zao wavivu
    Watukuzao upofu
    Ooo wanaumiza
    Ooo wanavunja moyo
    Wakatiza tamaa
    Lakini mimi, tazama
  3. Duniani kumbe siyo kwangu
    Nimetumwa kwa muda tu
    Nifanye kazi ya Bwana wangu
    Nimalize notoke tu
    Ooo nitaitimiza
    Ooo nimeamua
    Nikavalishwe taji
    Milele mimi, tazama
  4. Uchovu usingizi uvivu
    Na umaskini wangu
    Siruhusu vinitege nyavu
    Nishike utume wangu
    Ooo ninakaza mwendo
    Ooo sirudi nyuma
    Sitamwangusha Yesu
    Milele mimi tazama

    ~ ~ ~
    Kwa wanaomhitaji Yesu
    Nyimbo zake - kwa wanaomhitaji Yesu
    Habari zake - kwa wanaomhitaji Yesu
    Na kazi zake - kwa wanaomhitaji Yesu
    Mimi nayo nyumba yangu - nitamwimbia Bwana milele
    Na waimbaji wenzangu - nitamwimbia Bwana milele
    Mimi na rafiki zangu - nitamwimbia Bwana milele
    Ndugu na rafiki zangu - nitamwimbia Bwana milele
    Nitamwimbia Bwana milelee