Tumaini Jema

Tumaini Jema
Performed by-
CategoryGeneral
ComposerBernard Mukasa
Views2,731

Tumaini Jema Lyrics

  1. Hawataaibika, wala hawatafedheheka
    Milele na milele (milele) wao watashinda magumu
    Radi haitawapiga, mvua haitawagharikisha
    Milele na milele (milele) wao watashinda mauti

    Tazama
    Hawa ndio wale waliotambua (kuwa)
    Bwana Yesu ndiye fimbo ya ushindi (tena)
    Na wakakubali kumtumainia (yeye)
    Yesu ni mwamba na yeye mshindi (ni)
    Yesu kamanda wa wote tumwende yeye
  2. Wamtumainiao, wamechagua fungu jema
    Kwani hawatakwama wala kushindwa na lolote
  3. Yesu aliahidi, kutoa kila aombwapo
    Naye ni mwaminifu, anayetimiza ahadi
  4. Kuugua kufiwa, si tatizo kwa watu hawa
    Ufukara si hoja, kwa wamtumainiao Yesu
  5. Vita wameshavishinda, mapambano wamemaliza
    Na wamevikwa taji, wamevikwa taji la haki