Asante Yesu
   
    
     
         
          
            Asante Yesu Lyrics
 
             
            
- Ingawa ni Mungu na tena ni mfalme, umejinyenyekeza kwa wadogo sisi
 Ulishuka kwetu kukaa na sisi, unabaki kwetu daima katika Ekaristi
 
 Asante Yesu (aleluya) kwa wema wako (aleluya)
 Asante Yesu (aleluya) asante sana (aleluya)
 Kujitoa kwetu (aleluya) ukawa chakula, asante Yesu, asante sana
 Kujifanya kwetu (aleluya) kinywaji cha roho, asante Yesu, asante sana
- Tulapo mkate huu wa uzima, tunapata uzima tena wa milele
 Tunywapo kikombe hiki cha wokovu, twatangaza ufufuko wako uliye tukomboa
 
 Kila nikikutafakari, nikiwaza upendo wako kwangu nasema
 Asante Yesu asante,
 Yote unayonitendea, asilani siwezi elezea,
 Ee Yesu asante, Yesu asante
 Unatufundisha upendo, tuwajali wote wakubwa pia wadogo
 Asante Yesu asante
 Leo hii umetukuka, ninaomba nami unijaze baraka
 Asante Yesu Asante