Hima Hima Najongea

Hima Hima Najongea
Performed bySt. Francis of Assisi Kariobangi
AlbumZawadi Tosha
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerAlfred Ossonga
Views13,139

Hima Hima Najongea Lyrics

  1. { Hima hima leo, najongea kwako Bwana,
    Ninakuja kwako kwa unyenyekevu wangu,
    Nakuletea matunda ya jasho langu,
    Pokea Baba nami unipe Baraka } *2

  2. [ t ] Kwa ukarimu nimejitolea mimi mwenyewe,
    Polepole nasonga mbele nifike kwako,
    [ w ] Nikukabidhi nilicho nacho, hiki kidogo Baba pokea.
  3. Mapato yangu ni duni sana, we wanijua,
    Sina kitu kizuri cha kukuletea wewe,
    Nakukabidhi maisha yangu, uzima wangu Baba pokea.
  4. Mungu wangu ninakuja kwako nikushukuru,
    Umenilinda siku zote asante sana,
    Mavuno yangu nakupa wewe, na fedha zangu Baba pokea.
  5. Wiki nzima umenijalia uhai bure,
    Umenikinga na matatizo unanipenda,
    Mkate huu nakutolea, divai hii Baba pokea.
  6. Baraka zako ninazipokea siku kwa siku
    Mungu Baba nionyeshe Mbingu nifanye kazi,
    Mifugo yangu nakuletea, furaha yangu Baba pokea.