Mungu Baba Pokea

Mungu Baba Pokea
Alt TitleIpokee Sadaka Yetu
Performed bySauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerJoseph Makoye
VideoWatch on YouTube
Views25,464

Mungu Baba Pokea Lyrics

  1. Mungu Baba pokea sadaka yetu leo
    Tukutoleayo kwa jina la Mwanao
    Ya Abeli na Ibrahimu ilikupendeza
    Yetu Baba ipendeze uipokee

    Ipokee - (ipokee) sadaka yetu
    Ndilo fumbo - (ndilo fumbo) la kukupendeza
    La Baba na Mwana na Roho Mtakatifu *2
  2. Njooni wote tutoe sadaka yetu leo
    Kwa sifa na utukufu wake Mwenyezi
    Mkate huu na divai ndivyo mwili wake
    Kwa heshima kuu sadaka tumtolee
  3. Ee Mwenyezi tupokee tuwe mali yako
    Twakusihi kwa heshima utupokee
    Tunakutolea nguvu kazi na mavuno
    Kwa huruma yako dhambi tuondolee
  4. Kama mwanzo Mungu Baba a-si-fiwe
    Na mwanaye ndiye aliyetukomboa
    Roho Mtakatifu ndiye wetu mfariji
    Utatu Mtakatifu Mungu mmoja twakiri