Sasa Wakati Umefika

Sasa Wakati Umefika
Performed bySauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerBasil Lukando
VideoWatch on YouTube
Views52,376

Sasa Wakati Umefika Lyrics

  1. Sasa wakati umefika, wa kushika nilicho nacho (mimi)
    Kwa wema niende kwa Mungu nitoe zawadi
    Sasa wakati umefika kwenda mbele ya Mungu wangu (mimi)
    aone nilivyoandaa zawadi ya leo
    Nitamwambia Bwana pokea hiki kidogo nilichonacho
    Kwani Mungu wewe wanijua mimi siwezi hata kueleza
    Nakusihi sana Baba unipokee
    Nigawie na baraka niwe salama

  2. Mema yote niliyokuwa nayo yametoka kwa Mungu
    Hivyo nami ni kosa kusahau, kumshukuru
    Kwani kuwepo hapa leo hii ni kazi ya nani
    Kamwe mimi sitapata uwezo, pasipo Mungu
  3. Mema aliyotenda Mungu nijibu lini na vipi,
    Mbona hofu yazidi kuwa ndani, ya moyo wangu
    Mbele ya Bwana Mungu wangu kufanya siri ni bure
    Yeye ndiye mpanga mambo yote, ya wanadamu
  4. Pumzi inayonipa uhai inatoka kwa nani
    Bila Mungu hakika mwanadamu, siwezi kitu
    Nimepata nafasi ya leo ya kwenda kutoa zawadi
    Heri niende ya kesho sio yangu, ajua Mungu
  5. Ewe mwumba wa vyote duniani na vyote mbinguni,
    mimi leo nakuja kwako Baba, nihurumie.
    Baba we ndiwe unayetawala kulala na kuamka kwangu,
    Juu yangu utake nini Baba, kisifanyike.