Utukuzwe Ewe Baba

Utukuzwe Ewe Baba
Performed bySauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryOffertory/Sadaka
Composer(traditional)
VideoWatch on YouTube
Views41,466

Utukuzwe Ewe Baba Lyrics

  1. Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
    Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

    Utukuzwe - utukuzwe
    Baba Muumba ulimwengu - aleluya

  2. Tumepokea mkate, mazao ya mashamba, aleluya
    Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
  3. Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
    Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima, aleluya
  4. Zawadi ya divai, kutoka mzabibu, aleluya
    Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
  5. Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
    Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho, aleluya
  6. Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua, aleluya
    Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi, aleluya
  7. Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha, aleluya
    Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo, aleluya
  8. Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa, aleluya
    Na utukufu wako na kwa mafaa yako, aleluya