Utukuzwe Ewe Baba

Utukuzwe Ewe Baba
ChoirSauti Tamu Melodies
AlbumZilipendwa
CategoryOffertory/Sadaka
Composer(traditional)
VideoWatch on YouTube

Utukuzwe Ewe Baba Lyrics

  1. Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
    Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

    Utukuzwe - utukuzwe
    Baba Muumba ulimwengu - aleluya

  2. Tumepokea mkate, mazao ya mashamba -
    Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu -
  3. Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo -
    Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima -
  4. Zawadi ya divai, kutoka mzabibu -
    Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu -
  5. Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo -
    Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho -
  6. Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua
    Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi -
  7. Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha -
    Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo -
  8. Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa -
    Na utukufu wako na kwa mafaa yako -