Nikurudishie Nini Bwana
| Nikurudishie Nini Bwana | |
|---|---|
| Performed by | St. Monica Lower Kabete Campus UoN |
| Album | Uwe Nami Bwana |
| Category | Offertory/Sadaka |
| Composer | Evans Kibet |
| Views | 6,470 |
Nikurudishie Nini Bwana Lyrics
Nikurudishie nini - Mungu nirudishe nini
Mema mengi umenitendea, na mazuri mbalimbali
Sio afya (afya), sio mali (mali)
Si elimu (kweli) sio nyumba (Bwana)
Ninajiuliza kweli nirudishe nini x2- Kweli umenibariki katika maisha yangu,
Bwana mimi hivi nilivyo mbona nisikushukuru. - Tazama bomani ng'ombe, mbuzi nao kuku pia,
Wa kutaga wa kuuza, kweli nimebarikiwa. - Mvua inarutubisha, mimea inasitawi,
Maua ya kupendeza, aa yapendeza. - Watoto umenijalia, wana pia wajukuu,
Moyoni nina furaha, aa furaha tele.