Mpeni Kaisari

Mpeni Kaisari
Alt TitleVipaji Tumepewa
Performed byChrist The King Bungoma
AlbumPilka Pilka
CategoryOffertory/Sadaka
ComposerOchieng Odongo
Views31,620

Mpeni Kaisari Lyrics

  1. Vipaji tumepewa, mapato tumepata
    Lakini binadamu tunashindwa kushukuru
    Wakati tunaomba, tunajinyenyekesha
    Lakini tukipata mikono yetu birika

    Mpeni kaisari, yaliyo yake
    Mpeni Mungu (yale) yaliyo yake Mungu *2

  2. Mifugo tunafuga, nafaka tunavuna
    Lakini kila siku tunakula na kusaza
    Kumbuka kuna wale, wasio na chochote
    Hawawezi kupata, hata kikombe cha chai
  3. Tunapofanya kazi, twapata mishahara
    Shughuli zetu sisi kuingia kwenye baa
    Ikiwa zitabaki, twakuja kanisani
    Twamtolea Mungu, shilingi moja na tano
  4. Tukiwa na wagonjwa hatuwasaidii
    Wakati wamekufa tunachanga kwa huzuni
    Twachukua mikopo, kwa mambo ya anasa
    Ujenzi wa kanisa, twalazimishwa kutoa.
  5. Kumbuka Ibrahimu, alitoa mwanawe
    Kama sadaka kwake Mungu Baba wa mbinguni
    Na sisi kwa furaha, tupeleke zawadi
    Itakayopendeza, kama ile ya Abeli